Thursday 9 July 2015

Shukrani za Mh. Rais Kikwete kwa Mh. Edward Ngoyai Lowassa

Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Jakaya Mrisho Kikwete leo tarehe (9/7/2015) akiwa ndani ya bunge kwa ajili ya kulivunja bunge, pamoja na kutaja changamoto nyingi na mafanikio ya serikali ya awamu ya nne, Mh Jakaya Mrisho Kikwete alisema maneno yafuatayo

"Natambua kazi kubwa aliyoifanya Edward Lowassa kwa kipindi kifupi alipokuwa waziri mkuu wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, Namshukuru saana"


Haya ni maneno mazito saana na yenye dhamani saana kutoka kwa rais wa nchi yetu akitambua mchango wa rafiki yetu na mpendwa wetu Mh. Edward Lowassa, hivyo basi mchango na uchapakazi wa Edward Lowassa unajulikana na unatambulika saana na kueshimiwa pia. 4U Movement tunaye mtu wa kuipeleka nchi kwenye maendeleo ya kasi zaidi, maendeleo tunayoyahitaji, ambayo yatajengwa kwenye msingi wa sasa.

No comments:

Post a Comment

4U Movement wanakuomba kufuata maadili ya Kitanzania, Karibu !