Friday 12 June 2015

Mafuriko ya Tabora yafunika

mh. Lowassa ameendelea kuonyesha kuwa yeye ndo tegemeo na kiongozi anayehitajika kwa sasa Tanzania, hii imetokea mkoani Tabora baada ya watu wengi saana kujitokeza kutaka kumuona na kuzungumza naye. Pamoja na kuhitaji wadhamini 30 tu kila mkoa. Mh Lowassa jana amevunja record yake mwenyewe ya kupata wadhamini wengi baada ya kupata wadhamini zaidi ya 9000 mkoani Tabora, hii kweli inaonyesha watanzania wanamuhitaji kwa ajili ya maendeleo ya Tanzania

Mkoani Tabora, wananchi wamejitokeza kwa wingi saana kumdhamini mh. Lowassa na kuonyesha kuwa Lowassa ndo kipenzi chao

Misafara ya pikipiki ilikuwa mikubwa saana ikimkaribisha Mh. Lowassa


Foleni za kwenda kukutana na kumdhamini Mh. Lowassa zilikuwa kubwa saana, ila wana Tabora hawakuona shida kuhakikisha waafanikisha safari ya Matumaini

Mh.Lowassa akiwasalimia wananchi waliotaka asimame na kuwasalimia 


watu ni wengi saana, wanachama wa ccm na wasio wanachana woote wameungana katika kuhakikisha safari yetu ya matumaini inafanikiwa


Akina mama, vijana, wazee woote wakionyesha kuwa pamoja na mh. Lowassa katika safari ya matumaini

watu wakiendelea kumdhamini hm.Lowassa mkoani Tabora

1 comment:

4U Movement wanakuomba kufuata maadili ya Kitanzania, Karibu !